Home »
KITAIFA
» Wakulima wa zao la Karanga waiomba serikali kuwajengea viwanda vya kukamua mafuta.
Wakulima wa Karanga katika wilaya za Nanyumbu na Masasi Mkoani Mtwara wameiomba serikali kuwajengea viwanda vya kukamua mafuta ya ili kuongeza thamani ya zao hilo ambalo licha ya uzalishaji wake kuongezeka limeendelea kukosa soko kila mwaka na hivyo kusababisha baadhi ya wakulima kuacha kulima karanga.
Wakizungumza na Radio One Stereo iliyowatembelea baadhi ya wakulima wa karanga wamesema licha ya serikali kuwatumia watafiti kutoka Taasisi ya Kilimo Naliendele katika kuzalisha mbegu bora za zao hilo na kuonesha kufanya vizuri, bado masoko ni tatizo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dakta. OMAR MPONDA amesema mbegu zilizotafitiwa zimeonesha kufanya vizuri hivyo wakulima wanahitaji kusaidiwa.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nanyumbu Bwana HAMISI DAMUMBAYA amesema mazao mchanganyiko ikiwemo karanga yamefanikiwa kuiingizia halmashauri ushuru wa zaidi ya Shilingi Milioni Mia-Tatu na kusisistiza halmashauri iko katika harakati za kutafuta masoko.
Related Posts:
Siku Tatu za Hatma ya Lowassa PolisiZIMEBAKI saa 72 kuanzia leo zenye umuhimu mkubwa kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.Hali hiyo inatokana na taarifa kuwa kiongozi huyo ataripoti polisi siku ya Alhamisi ambako huko itajulikana kama ataendelea kuhojiwa n… Read More
Rais Magufuli Awataja Waliotengeneza Maisha yake ya Kisiasa Hadi Kuwa KiongoziRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amesema kuwa Marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete ndio waliotengeneza maisha yake ya kisiasa hadi kuwa kiongozi.Rais Magufuli ameyasema hayo Jumata… Read More
Mwanaume Auawa kwa Risasi Kibiti......Mwanamke Ajeruhiwa kwa RisasiWatu wasiojulikana wanadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi, mkazi wa Kijiji cha Ruaruke, wilayani Kibiti, Mkoa wa Pwani Ramadhani Mzurui, usiku wa kuamkia leo.Kadhalika watu hao walimjeruhi mguuni kwa risasi mke wa marehemu.Mgang… Read More
RC GODFREY ZAMBI awasimamisha kazi watumishi sita wa vitengo mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi.Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bwana GODFREY ZAMBI amewasimamisha kazi watumishi sita wa vitengo mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi ili kuruhusu kufanyika kwa uchunguzi kutokana na utendaji wao usioridhisha.… Read More
Mkapa: Wale Niliowaita Wapumbavu, Kwa Maendelea Haya Sekta ya Afya Naamini 'Upumbavu' Wao UtapunguaRais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa amefunguka na kusema tafiti zilizotolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Ally Mwalimu zitawafungua kidogo wale watu aliowaitawapumbavu… Read More
0 comments:
Post a Comment