Wakizungumza na Radio One Stereo iliyowatembelea baadhi ya wakulima wa karanga wamesema licha ya serikali kuwatumia watafiti kutoka Taasisi ya Kilimo Naliendele katika kuzalisha mbegu bora za zao hilo na kuonesha kufanya vizuri, bado masoko ni tatizo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dakta. OMAR MPONDA amesema mbegu zilizotafitiwa zimeonesha kufanya vizuri hivyo wakulima wanahitaji kusaidiwa.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nanyumbu Bwana HAMISI DAMUMBAYA amesema mazao mchanganyiko ikiwemo karanga yamefanikiwa kuiingizia halmashauri ushuru wa zaidi ya Shilingi Milioni Mia-Tatu na kusisistiza halmashauri iko katika harakati za kutafuta masoko.
0 comments:
Post a Comment