Home »
Kimataifa
» Hofu yatanda katika bandari Marekani kufuatia tishio la kuwepo kwa bomu
Walinzi wa pwani katika bandari ya Charleston upande wa South Carolina Marekani walilazimika kuondoa maafisa wa mamlaka ya bandari hiyo na wafanyakazi kufuatia ilani ya kuwepo kwa bomu katika mojawapo ya shehena .
Maafisa wa uslama wa pwani walifahamisha kwamba kuliwa na ilani ya kuwa na bomu katika meli ya Maersk Memphis iliyokuwa imeegeshwa katika bandari hiyo.
Tukio hilo limeripotiwa kutokea siku ya Jumatano majira ya jioni saa mbili na baada ya wafanyakazi kuondoka bandari hiyo walinzi walianza uchunguzi mara moja .
Meli hiyo inasemekana ilikuwa imetoka nchini Pakistan.
Baadaye idara ya ulinzi wa pwani kupitia twitter walifahamisha kwamba bandari hiyo ipo salama na kwamba hamna tishio lotote la bomu.
Related Posts:
Historia ya Che GuevaraKama kijana msomi wa shahada ya udaktari, che Guevara alisafiri nchi nyingi sana huko bara la Amerika ya kusini na rafiki yake, akawa ni mtu mwenye uchungu mkubwa kuona maisha ya dhiki,njaa, magonjwa nchi za America ya kusini… Read More
JOSEPH KABILA Tutaendelea kuzungumzia hali ya kisiasa kufikia muafaka Afrika Kusini imeitaka serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC pamoja na wanasiasa wa upinzani kuendeleza mazungumzo yenye lengo la kupata muafaka wa kisiasa katika taifa hilo.Rais Jacob Zuma ametoa rai h… Read More
Nyuki ‘wamlazimisha’ mshukiwa kujisalimisha KenyaTaarifa kutoka magharibi mwa Kenya zinasema kuwa mtuhumiwa wa wizi wa gari alijisalimisha kwa polisi baada ya kuvamiwa na nyuki akiliendesha gari hilo.Mwandishi wa BBC, Wanyama wa Chebusiri kutoka Nairobi, anasema ripoti hiyo… Read More
Waliomuingiza mtu mweusi kwenye jeneza, Mahakamani Afrika KusiniHatimaye wakulima wawili weupe wanatarajiwa kufikishwa mahakamani nchini Afrika Kusini, kwa tuhuma za kumsukuma mtu mmoja mweusi na kumuingiza ndani ya jeneza, huku wakitishia kummwagia mafuta ya petroli ili kumteketeza kwa m… Read More
China yaanza kuzipatanisha Afghanistan, PakistanRais Ashraf Ghani na Waziri wa Mambo ya Nje Wang Yi.… Read More
0 comments:
Post a Comment