Washtakiwa hao Willem Oosthuizen na Theo Jackson, walikamatwa Novemba mwaka jana, baada ya video ya kitendo hicho kuzungushwa mitandaoni.
Walisema kuwa, Victor Mlotshwa alipita kwenye shamba lao lililopo katika jimbo la Mpumalanga, bila ya kuwa na idhini, na kwamba hatua waliyochukuwa ilikuwa ni kumuadhibu.
Katika kusikilizwa kwa kesi hiyo awali, Jaji wa mahakama alisema kuwa wakulima hao walikuwa ni wakatili na waliojaa tabia za ubaguzi wa rangi.
0 comments:
Post a Comment