Akizungumza mara baada ya kutembelea kiwanda hicho ambacho kinatengeneza badhaa aina ya mikeka kwa kutumia betry zilizotumia amesema serikali hii inatoa kipumbele kwenye uendelezwaji wa viwanda hasa vinavyouza bidha nje ya nchi lakini pia wanasisitiza viwanda hivyo vifuate sheria ili uwekezaji huo usilete madhara.
Amesema viwanda vinatakiwa kutoa taarifa ya ubora wa hewa kila baada ya miezi mitatu kwa baraza la mazingira NEMC hivyo ametoa muda wa siku 15 na kuwashauri wenye kiwanda hicho kuangilia uwezekano wa kufanya mazungumzo na wenye nyumba ziliojirani kabisa na kiwanda hicho pamoja na serikali ili kuangalia uwezeko wa kununua nyumba hizo.
Nae Ofisa Mhakiki wa kiwanda hicho Bw Ankleti Pereira amesema hilo ni eneo la viwanda na kwamba swala la moshi haliepukiki kwenye viwanda.
0 comments:
Post a Comment