Ikiwa ni operesheni ya kawaida zinazofanywa na jeshi la polisi wilaya ya Lindi na ushirikiano wa raia wema, kikosi maalum kilifanya msako katika kijiji cha Mnali na kufanikiwa kukuta shamba lililosheheni miche ya bangi.
Jeshi la polisi likiongozwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi mwandamizi,Renatha Mzinga pamoja na kufuata taratibu za kisheria , waliteketeza shamba hilo.
Kwa mujibu wa sheria , Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Lindi Erasto Yakobo Phili alishuhudia uwepo wa shamba hilo na kuamuru kuteketezwa.
0 comments:
Post a Comment