Friday 8 June 2018

Waraka wa KKKT....Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini Asimamishwa Kazi.



DAR: Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Idara ya Sheria na Usajili wa Jumuiya za Kidini na Vyama vya Kijamii, Merlin Komba

Bi. Merlin amesimamishwa leo Juni 08 ili kupisha uchunguzi wa barua iliyoandikwa kwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT)

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT) liliandikiwa barua kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia kwa Msajili wa Vyama na kupewa siku 10 kufuta Waraka wake

0 comments:

Post a Comment