Friday 16 March 2018

BAADA YA KUITOA AC MILAN EUROPA LEAGUE, WENGER AHOFIA KUKUTANA NA ATLETICO, KAYASEMA HAYA



Baada ya Arsenal kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya AC MIlan usiku wa jana kwenye hatua ya 16 ya Europa League, Kocha Arsene Wenger amesema hahitaji kukutana na Atletico Madrid.

Atletico na Arsenal zimefuzu kuingia hatua ya nane bora ya michuano hiyo huku droo ya timu zitakazokutana robo fainali ikitaraji kufanyika kesho.

Wenger amesema anatamani kutokupangwa na timu hiyo ya Spain ili aweze kupata unafuu wa kupenya kwenye mashindano hayo.

Aidha Wenger amesema kuwa wamekutana na wakati mgumu katika mechi zilizopita hivi karibuni na hatimaye wamekuja kupata matokeo kwenye michezo ya mwisho.

Arsenal imefuzu kuingia hatua hiyo baada ya kuifunga AC Milan kwa jumla ya mabao 5-1.

0 comments:

Post a Comment