Zitto ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa facebook mara baada ya kutokea taarifa ya kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu na watu wasiyofahamika.
"Mbunge mwenzetu wa Singida Mashariki amepigwa risasi nyingi na watu wasiojulikana. Kakimbizwa hospitali Dodoma.
Nchi yetu imefungua ukurasa mpya. Wananchi tusimame imara tusikubali Kabisa kuingia kwenye siasa za namna Hii. Mola amponye ndugu yetu", ameandika Zitto.
Mhe. Tundu Antipas Lissu amepigwa risasi kadhaa mwilini mwake akiwa nyumbani kwake Dodoma eneo la 'area D' na watu wasiojulikana.
0 comments:
Post a Comment