Ametoa shukrani hizo kwa niaba ya familia yake na kuongeza kuwa Watanzania wote wanastahili pongezi hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake Kunduchi Dar es Salaam leo, amesema kabla hajarejea ofisini kwake mjini Dodoma anawashukuru wananchi wote.
Shukrani hizo zimelenga Watanzania wote kwa ujumla wakiwepo wakazi wa Kyela alipozikwa mke wake, makanisa mbalimbali likiwemo kanisa la Moravian, Mashkeh akiwemo Mufti Mkuu na madaktari wote waliohusika kumsaidia marehemu.
Shukrani zingine alizitoa kwa wamiliki wa vyombo vya habari , watangazaji na waandishi wote wa habari waliofuatilia tangu ulipotokea msiba huo.
0 comments:
Post a Comment