Saturday, 1 July 2017

Wananchi elfu moja wa kijiji cha Katambike wanatarajiwa kukosa makazi yao


Zaidi ya Wananchi elfu moja wa kijiji cha Katambike halmashauri ya Nsimbo wilayani mpanda mkoani Katavi wanatarajiwa kukosa makazi yao baada ya nyumba zao kuwekewa alama ya X na shirika la Reli na kuwapatia siku 30 za kubomoa nyumba hizo.

Wakizungumza na kituo hiki wakazi wa kata ya Ugalla wamesema wanaiomba serikali iweze kuwaongezea muda wa kuhama katika eneo hilo na kuiomba halamshauri ya Nsimbo kuweza kuwaandalia eneo la makazi huku wakidai huduma ya afya maji na shule.

Baadhi ya wakazi hao wanatoa lawama kwa mwenyekiti wa kijiji na afisa mtendaji kwa kuwaambia watoe kiasi cha shilingi elfu hamsini kwa ajili ya kuwapimia maeneo ya kuishi huku maeneo hayo hayajapimwa.

Kwa upande wake diwani wa kata hiyo ameiomba serikali iweze kuongeza siku na kuiomba halmashauri hiyo kujenga shule na kituo cha afya na hapa anasema.

0 comments:

Post a Comment