Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka amesema kauli ya Mzee Mwinyi imetokana na utendaji wa kuvutia na uchapakazi mzuri wa Rais Magufuli na ni maoni yaliyotolewa wazi bila kushurutishwa na mtu bali ni mawazo yake kama Mtanzania.
“Ni ukweli usiofichika kwamba maoni ya Mzee Mwinyi bila shaka yoyote yameenda moja kwa moja kutokana na kuvutiwa na uchapakazi wa Rais Magufuli. Pia maoni hayo hayakuwa ni uwamuzi wala kushurutishwa na mtu bali ni mawazo yake kama Mtanzania na kama Mwananchi mwingine.
“Maoni ya Mzee Mwinyi yalikuwa bayana au unaweza kusema mubashara yanayoweza kumlazimisha kila binadamu mwenye akili timamu hafahamu kwa kila alichotamka katika matamshi yake. Alichokisema ni jambo lenye mantiki baada ya kuaangalia hatma ya Taifa na uzalendo wa Taifa.” – Shaka Hamdu Shaka.
0 comments:
Post a Comment