Akizungumza na Madiwani wa Halmashauri hiyo Zambi amewataja waliosimamishwa kuwa ni Wakuu wa Idara za Sheria inayoongozwa na NYAMANDE KASIMIR,Mkaguzi wa Ndani, Bwana IDD MBOWETO, Mtunza Hazina, Bwana GERVAS NGOMANO, Kaimu Mhandisi wa Ujenzi Bwana ASWILE MWASAGA, Bwana HAROUN KINAWA wa Ushirika pamoja na Bwana DANIEL KASEMBE ambaye anakaimu kitengo cha Ugavi katika Halmashauri hiyo.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa wafayakazi hao wameshindwa kuzijibu hoja 36 ambazo zimebainika na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali- CAG, zikiwemo kutofuatilia madai ya muda mrefu ya Shilingi Milioni 669 na Laki- 6, kutosimamia makusanyo ya mapato ya madeni kutoka AMCOS mbalimbali yanayofikia Shilingi Milioni 127 na Laki- 8 na kufanya mikataba bila kuzingatia taratibu.
Kutokana na hali hiyo Bwana ZAMBI amemwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bwana RAMADHAN KASWA kuunda tume ya kuchunguza tuhuma za watumishi hao na watakaobainika kuwa na makosa hatua za nidhamu zitachukuliwa dhidi yao.
0 comments:
Post a Comment