Thursday, 20 July 2017

Kiongozi wa upinzani Zambia alalamikia mateso gerezani


Kiongozi wa upinzani nchini Zambia aliye korokoroni Hakainde Hichilema, amefikisha siku 100 gerazani tangu akamatwe akilalamikia mazingira mabaya yaliyo gerezani.

Alikamatwa baada ya msafara wake kukataa kuupisha ule wa rais

Anakabiliwa na mashtaka uhaini kufuatia kisa hicho.

Bwana Hichilema ambaye kwa sasa anazuiliwa katika gereza lenye ulinzi mkali, aliandika kwenye mtandao wake wa Facebook kuwa hana chuki na yeyote 

Alisema mapenzi yake ni kuona mabadilko nchini Zambia.

"Tunaamini kuwa licha ya wafungwa hawa kufanya makosa, wanahitaji kuhudumiwa kwa njia ya kibinadamu," alisema hichilema.

0 comments:

Post a Comment