Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Nyamisi Bahati (27) anayedaiwa kumuua mtoto wake aitwaye Sakimu Hassani baada ya kumtupa ziwa Victoria na kupelekea mtoto huyo kupoteza maisha, tukio analodaiwa kulifanya majira ya saa 1:00 usiku ya tarehe 13/06/ 2017.
Inadaiwa mtuhumiwa ambaye ni mama wa mtoto huyo alitoka nyumbani kwa mumewe na kwenda kuwasalimia wazazi wake akiwa na mtoto wake, lakini baadaye alitoka nje akiwa na mtoto kama anakwenda kumbembeleza ndipo baada ya muda kupita alirudi akiwa hana mtoto na kupelekea Mama yake mzazi wa binti huyo kumuuliza mtoto amemuweka wapi ndipo mtuhumiwa alionekana na mashaka huku akishindwa kuonyesha mahali mtoto alipo na baadaye akasema amemtupa kwenye Ziwa Victoria.
Kamanda Msangi amesema baada ya mtuhumiwa kusema hivyo, Bibi wa mtoto alipiga yowe akiomba msaada kwa watu ili waweze kuja kumuokoa mtoto na wananchi walipofika waliweza kutoa taarifa kituo cha Polisi na kuweza kufika eneo la tukio ambapo walishirikiana na wananchi na kufanya kazi ya kumtafuta majini na baadaye walifanikiwa kumpata ila alikuwa tayari ameshapoteza maisha.
Kamanda Msangi ameendelea kusema kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha mtuhumiwa wa mauaji hayo anasumbuliwa na matatizo ya akili, japokuwa Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
Wednesday, 14 June 2017
Mwanza: Mwanamke amtupa mtoto ziwani
Related Posts:
Kilichojiri baada ya Lowassa kufika kuhojiwa na DCIWaziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Edward Lowassa leo July 20, 2017 ameripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai kuhojiwa ‘DCI’ kuhojiwa kwa mara ya nne.Lowassa ametakiwa kurudi t… Read More
Wanaotapeli Watalii, Ujumbe huu uwafikieWaziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amesema atapambana na matapeli wote ambao wamekuwa wakiuza safari za watalii kwa njia ya mtandao.Amesema kumekuwepo na malalamiko yanatolewa na baadhi ya watalii kuwa wa… Read More
KIMENUKA...Mbunge Saed Kubenea Aitwa Polisi.......Mbunge wa jimbo Ubungo,(CHADEMA) Saed Kubenea ameitwa polisi na kutakiwa kuripoti leo tarehe 20/7/ 2017 kutoa maelezo kituo cha polisi kufuatia malalamiko aliyotoa Profesa Lipumba Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili w… Read More
WARUNDI Mrudi Nchini Kwenu Hapa sio Kwenu- Rais MagufuliRais John Magufuli amewataka wanachi wenye asili ya urundi waliopo nchini Tanzania wafanye wawezavyo kwa hiari yao warudi kwao wakaijenge nchi wasisingizie kuna vita kwa kuwa Rais wao Pierre Nkurunziza ameshawahakikishia kuwa… Read More
Rais Magufuli Aagiza milioni 200 za mradi wa maji jeshini zitumike kwa wananchiRais John Magufuli ameagiza Sh200 milioni zilizopangwa kutumika katika mradi wa maji katika kambi ya jeshi zianze kuimarisha miradi ya maji kwa wananchi kwanza.Akizungumza leo, Alhamisi Julai 20 katika ziara … Read More
0 comments:
Post a Comment