Sunday 18 June 2017

WARIOBA :Msaidieni Rais tushinde Vita ya Rasilimali za nchi, Suala la Makinikia sio la Chama wala Siasa ni la Watanzania wote



Wananchi hawahitaji mgawanyiko wa uongozi na malumbano wanataka maendeleo.Msaidieni Rais tushinde Vita ya Rasilimali za nchi 
Suala la Makinikia sio la Chama wala Siasa ni la Watanzania wote 

Hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli alipokea ripoti ya Kamati ya kwanza na ya pili ya uchunguzi wa makontena 277 ya mchanga wa madini (makinikia) yaliyokuwa njiani kusafirishwa nje ya nchi na uchunguzi ulifanyika na kulibaini ndani ya mchanga huo kuna dhahabu na madini mengine kwa asilimia kubwa. 

Aidha, Mhe Rais amechukua hatua mbalimbali kulingana na ushauri wa kamati husika, pamoja na maamuzi yake kama Rais. Kutokana na sakata la hilo, Idara ya Habari-MAELEZO imepata fursa ya kufanya mahojiano na Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mstaafu Mheshimiwa, Jaji Joseph Sinde Warioba katika ofisi zake zilizopo Osterbay Jijini Dar-es-salaam. 

SWALI: Ninanukuu maneno ya Baba wa Tafa, Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere kuhusu raslimali za nchi na hususan madini alisema: “Madini yetu tuliyonayo ni vema kuyaacha mpaka Watanzania watakapokuwa na ufahamu wa kutosha wataamua kuyachimba” mwisho wa kunukuu nini maana yake? 

JIBU: Mara baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 Hayati, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipokea nchi kama Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru akiwa hana wataalamu zaidi ya madaktari 2 na yeye mwenyewe ambaye alikuwa msomi kutoka chuo Kikuu cha Edinburg Uingereza. Kwa hali hiyo, Mwalimu alikuwa sahihi usingeweza kuruhusu rasilimali za nchi mfano madini kuchibwa na wageni kutoka nje maana yake Watanganyika wangekuwa watazamaji tu bila kufaidika na lolote. 

Mwalimu alihakikisha anawekeza katika elimu ambayo ilikuwa bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu elimu ndio msingi wa kuondoa Ujinga Umasikini na Maradhi. Alitambua Watanganyika wakielimika na kupata utaalamu wa madini ikiwani pamoja na uchimbaji watakuja kuyachimba na kufaidika. 

SWALI:Tanzania ni kati ya nchi zilizobarikiwa kuwa na raslimali nyingi za kila aina kuanzia madini, gesi, wanyamapori na hifadhi, misitu, milima, maporomoko ya maji, mabonde maziwa makubwa kwa madogo, bahari ya hindi na raslimali za mazao ya uvuvi, nchi yenye ardhi ya kutosha watanzania wenye uwezo wa kufanyakazi kwa ufanisi . Unadhani nini tatizo letu, nini cha kufanya? 

0 comments:

Post a Comment